FAHAMU DALILI ZA UGONJWA WA MAFUA MAKALI YA NDEGE

ByChengula

Jun 12, 2021

Huu ni ugonjwa hatari sana kwa kuku na jamii nyingine za ndege pia hupata binadamu

Husababisha vifo vingi sana vya ndege na binadamu wakipatwa huweza kufa pia.

 

MAAMBUKIZI

 

Ugonjwa huambukiza kwa njia ya hewa, hewa, maji, kugusana, macho, midomo, na pua.

 

DALILI ZA UGONJWA

 

Dalili nyingi za Mafua ya ndege hufanana na ugonjwa wa kideri

 

JINSI YA KUDHIBITI UGONJWA

 

— Hakuna matibabu

— safisha Mabanda

— kunawa vizuri Baada ya kushika mzoga wa kuku aliekufa kwa ugonjwa

— kaa mbali na mizoga iliyokufa kwa ugonjwa

— tenganisha kuku wazima na wagonjwa

— fukia au choma mizoga ya kuku

— usiuze au kununua kuku wagonjwa

— usile kuku mgonjwa au aliekufa

— tenganisha kuku wageni na wenyeji kwa muda wa wiki 2

–toa taarifa ofisi ya mifugo unapoona dalili za ugonjwa

 

ANGALIZO

 

Mafua makali ya ndege mpaka sasa hayajawahi kuingia TANZANIA

Hata hivyo tunatakiwa kuwa waangalifu tunapoona ugonjwa wa Mafua ukiwapata aina tofauti ya jamii ya ndege pamoja na binadamu kwa wakati mmoja.

Kama tukiona hivyo tunatakiwa kutoa taarifa ofisi ya mifugo haraka..

Leave a Reply