Huduma za ugani zinazotolewa na watalaam wa mifugo

Huduma za ugani hutolewa na wataalam wa mifugo wa Serikali wa Halmashauri, pamoja na sekta binafsi katika kliniki na vituo vya mifugo.

 

Huduma zinazotolewa na Wataalamu wa Mifugo wa Serikali:-

  1. Kutoa tiba na kinga dhidi ya magonjwa ya mifugo
  2. Kutoa elimu na ushauri kwa wafugaji kuhusu kanuni za ufugaji bora
  3. Uhamilishaji (A.I.) na kupima mimba
  4. Ukaguzi wa nyama na ngozi
  5. Kutoa vibali vya kusafirisha mifugo
  6. Kutoa vibali kwa watu walioumwa na mbwa/wanyama kuweza kupata chanjo ya kuzuia ugonjwa wa kichaa cha mbwa katika hospitali za binadamu.

 

Huduma zinazotolewa na wataalam wa sekta binafsi:

  1. Kutoa tiba na kinga dhidi ya magonjwa ya mifugo
  2. Kutoa elimu na ushauri kwa wafugaji kuhusu kanuni za ufugaji bora
  3. Uhamilishaji (A.I.) na kupima mimba

Leave a Reply