Kuharisha damu kwa kuku (coccidiosis):

Kuku wanaopata lishe bora, kutunzwa vizuri na kupatiwa chanjo dhidi ya magonjwa yanayotokea mara kwa mara huwa na afya nzuri. Ni bora kuzuia magonjwa kuliko kutibu ili kupunguza vifo na gharama. Iwapo ugonjwa utatokea kuku wagonjwa watenganishwe na kuku wasio wagonjwa na wapatiwe tiba. Kanuni muhimu za kufuata ili kuzuia magonjwa ni:-

  • Banda liwe safi muda wote,
  • Kabla ya kuweka kuku, banda linyunyiziwe dawa ya kuua wadudu wa magonjwa mbalimbali,
  • Kuku wakaguliwe kila siku ili kubaini wagonjwa au wenye matatizo, kuwatenga na kutoa taarifa kwa mtaalam wa mifugo,
  • Kuku wapatiwe chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali,
  • Watu wasiohusika wasiingie eneo la kufugia kuku bila utaratibu,
  • Ndege na wanyama wengine wasifike eneo la kufugia kuku,
  • Banda la kufugia kuku litenganishwe na mabanda ya mifugo mingine,
  • Lango la kuingilia katika banda la kuku liwekewe dawa ya kukanyaga kwa wanaoingia ndani ili kuzuia kuingiza vimelea vya wadudu wa magonjwa; na
  • Vifaa vya chakula na maji viwe safi wakati wote.

 

DALILI ZA KUKU MGONJWA

Dalili za ujumla zinazoonekana kwa kuku mgonjwa ni kama zifuatazo:-

  • Kuzubaa,
  • Kupoteza hamu ya kula,
  • Kujitenga na wenzake katika kundi; na
  • Kupunguza au kusimama kutaga.

Mfugaji anapoona mojawapo ya dalili hizo amwone mtaalam wa mifugo

 

SOMA PIA MAGONJWA YA KUKU -ORODHA YA MACHAPISHO

Leave a Reply