Ufugaji wa kuku tangu vifaranga

ByChengula

Sep 26, 2015

ULEAJI BORA WA VIFARANGA

Mambo mengi yanayohusika katika uleaji wa vifaranga kwa upande wa HARSHO FEEDS tupo tayari kumhudumia mfugaji wa kuku kwa kumpatia chakula na utaalamu sahihi. Katika uleaji wa vifaranga kuna tofuati kati ya vifaranga wa nyama na wale wa mayai hasa katika chanjo na lishe.

 

MATAYARISHO

Banda la kuku liwe imara kuepuka wizi, panya, ndege, nyoka na kadhalika. Jenga sehemu yenye hewa ya kutosha, kavu na mbali na kuku wengi.

Kabla ya kuingiza kuku, safisha banda lote nje na ndani kwa dawa ya kuangamiza wadudu. Paka chokaa kwenye kuta zote. Hakikisha banda haliwi na joto kali, baridi, kuingiwa na mvua, jua au upepo.

Tayarisha chakula bora, maji safi, madawa-vifaa vya kutosha na tandiko safi.

 

KABLA YA KUFIKA VIFARANGA

Banda la kuku liwe tupu wiki moja hadi mbili baada ya kusafishwa na dawa. Vifaranga utakaopokea wawe na historia nzuri.

a)   Usichanganye vifaranga wa sehemu tofauti

b )  Tengeneza mduara ndani ya banda kwa kutumia hardboards kwa urefu wa sentimeta 50 na katikati yake weka taa ya (balbu) au jiko la mkaa, hakikisha mwanga wa kutosha ili vifaranga waone chakula na maji.

c)  Weak tandiko la kuku (litter) safi, vifaa vya maji na chakula kulingana na idadi ya vifaranga.

d)   Masaa matano kabla ya vifaranga hawajafika washa taa za joto au jiko la mkaa kwa ajili ya kutoa joto kwa vifaranga (35oc) weak maji ndani ya vyombo ili yawe na joto kiasi. Hakikisha kuna hewa ya kutosha na hakuna upepo unaoingia.

e)   Iwapo vifaranga vinatoka mbali na vimechoka, weka glucose/sukari kidogo kwenye maji (kijiko cha chakula kwa lita tano za maji)

 

KUPOKEA VIFARANGA

Watoe vifaranga kwenye maboksi na kuwaingiza ndani ya mduara, hakikisha unayo hesabu kamili.

Vifaranga wote wanywe maji na uwanyweshe ambao hawajakunywa maji. Baada ya masaa mawili, weka chakula kwenye vyombo vya chakula.

Hakikisha kuna mwanga masaa 24 kwa siku tano za mwanzo na joto la kutosha.

Hakikisha kuku wana nafasi ya kutosha. Panua duara la kuelekea kadri kuku wanavyokuwa na ondoa duara baada ya wiki tatu. Kuku wakibanana hawakui vizuri kwa kipindi hiki.

 

ULEAJI KUKU MAYAI (Layers)

Kila kuku anayetaga apate eneo la futi mbili (2) za mraba. Nyumba iwe na madirisha ya kutosha kuweza kuingiza hewa safi. Tumia kati ya vitu vifuatavyo kwenye sakafu kama godoro (litter):-

a)  Maranda ya mbao

b)  Maganda ya mpunga

c) Majani makavu yaliyokatwakatwa

 

VIFAA

Weka vifaa vya kutosha kulishia chakula na maji kwenye banda lako kama ifuatavyo.

Sinia moja litumike kulishia vifaranga 50. Vifaa vya maji tumia

Chick Fount moja kwa vifaranga 100.

Kuku wakubwa tumia “Feeder” moja kwa kuku 50 na drinker moja kwa kuku 60

 

CHAKULA KINACHOTAKIWA

Umri (wiki) Aina ya chakula
0-4 Chick Starter
5-8 Chick Mash
9-20 Growers Mash
21-89 Layers Mash

 

UMRI

(wiki)

CHAKULA

(Grams)

MAJI (ml) WASTANI

WA UZITO (grams)

1 12 13 20-30 50
2 19 20 40-50 100
3 25 25 50-50 150
4 30 29 60-70 200
5 35 33 70-80 300
6 40 37 80-100 400
7 45 41 100-120 500
8 50 46 120-130 650
9 54 51 130-140 800
10 60 56 150-160 900
11 67 61 160-165 1000
12 65 66 165-170 1100
13 68 73 170-175 1200
14 71 77 175-180 1300
15 74 75 180-190 1400
16 76 77 190-195 1500
17 78 80 195-200 1600
18 80 86 20-210 1700
19 83 95 210-220 1750
20 86 100 220

 

Katika kilele cha utagaji kuku mmoja anahitaji gram 120-135 kila siku hii ni sawa na kilo 12 – 12/siku/kuku/100. kiasi hiki kinategemea ubora na lishe ya kuku unachotumia.

 

MPANGO WA KUBADILI CHAKULA

Unapobadili chakula usibadili ghafla. Badili chakula kutoka Chick Starter hadi Growers Mash na Growers Mash hadi Layers Mash kwa mpangilio ufuatao.

½ Chick Starter + ½ Growers Mash changanya vizuri na lisha kwa wiki moja. Kisha endelea na Growers Mash fuata utaratibu huo utakapobadili Growers kwenda Layers

 

UMRI (siku/wiki) Aina ya chanjo Njia ya kuwapa
Siku 1 Markers Sindano Hatchery
Siku 7 New Castle-lasota Maji ya kunywa
Siku 14 Gumboro Maji ya kunywa
Siku 21 Gumboro Maji ya kunywa
Wiki 8 – 10 New Castle Maji ya kunywa

 

 

MPANGO WA KINGA – KUKU WA MAYAI

CHAKULA KINACHOHITAJIKA Umri (Wiki)            

 

 Aina ya chakula

0-3                           Broiler Starter

4-8                           Broiler Finisher

UMRI (wiki) CHAKULA (grams) MAJI (ml) WASTANI WA UZITO (grams)
1 20 40-50 130-150
2 30 60-80 260-300
3 50 100-120 460-520
4 70 140-160 750-800
5 90 180-200 1000-1200
6 105 210-230 1300-1500
7 115 230-280 1600-1800
8 120 240-300 1900-2100

 

 

Rudia chanjo ya New Castle kila baada ya miezi 3-4, chanjo ya Mareks hufanyika Hatchery kabla ya mfugaji kupewa vifaranga.

 

SIFA ZA KUKU BORA WA MAYAI

Kuku waliotunzwa vizuri tegemea yafuatayo:-

ª   Vifo wakati wa kulea 3% – 5%

ª   Vifo wakati wa utagaji 1% kwa mwezi

ª   Umri wa kuanza kutaga wiki 19-20

 

TIBA YA MINYOO

Hii hufanyika kwenye kuku wa mayai:

Mara ya kwanza wapewe wiki ya 8 kurudiwa ya 18

Baada ya wiki 18 wasipewe tena na dawa ya minyoo hadi baada ya kupitia kiwango cha juu cha utagaji (peak production)

Baada ya Peak Production kuku wapewe dawa ya minyoo kila baada ya wiki 8-10 au minyoo inapoonekana kwenye kinyesi

 

KUKU WA NYAMA (BROILERS)

Kila kuku wa nyama anapaswa apate eneo la futi moja (1) ya mraba. Nyumba iwe na madirisha ya kutosha, hewa safi, sakafu iwe na godoro (litter) ya randa au maganda ya mpunga.

 

VIFAA

Vifaranga 100 wanaweza kutumia chombo kimoja cha kulishia

(chick plate) na chombo kimoja cha kunywea maji (chick fount) kwa wiki moja kuanzia wiki ya pili na kuendelea tumia chombo kimoja cha kulishia (feeder) chenye kipenyo cha sentimenta 38 kwa kuku 50 .

 

 

MPANGO WA KINGA – KUKU WA NYAMA

UMRI (siku/wiki) AINA YA CHANJO NJIA YA KUWAPA
Siku 7 New Castle Maji ya kunywa
Siku 14 Gumboro Maji ya kunywa
Siku 21 Gumboro Maji ya kunywa

 

Muhimu Zingatia

Fuata ratiba ya chanjo kama ilivyopendekezwa

Pata chanjo toka sehemu inayojulikana na yenye uhakika wa upatikanaji

Hifadhi chanjo yako kwenye fridge na sio freezer sehemu yenye nyuzijoto 4 – 8 centigrade.

Chanjo isitolewe zaidi ya saa 4.30 asubuhi kwa sababu chanjo inaweza kuharibika kutokana na joto au mwanga mkali wa jua.

 

Unapoona dalili za ugonjwa, kama kusinzia, kujikunyata, kuharisha, kutokula chakula, kutokunywa maji, kuhema kwa tabu au vifo, toa taarifa haraka kwa mtaalamu wa mifugo ili upate ushauri na huduma mara moja.

 

Jarida hili limetayarishwa na HARSHO TRADING CO. LTD

Head Office: Kawawa street. Moshi. Branch: Along Moshi Arusha Rd. Bomang’ombe P.O. BOX 810.

Moshi, Tanzania

Tel: 0784 287409 / 027 2753503

Fax: +255 27 2753505

E-mail: harshotrad@yahoo.com

Website:- www.harshotz.com

Leave a Reply