Aina za mabwawa ya kufugia samaki

Aina za mabwawa ya kufugia samakiBwawaAina za mabwawa ya kufugia samaki

MABWAWA YA KUFUGIA SAMAKI

 Bwawa1
Hili ni bwawa la kuchimbwa chini, lipo katika kituo cha ufugaji wa samaki cha serikali kilchopo Kingolwira mjini Morogoro. Yapo na mabwa mengine mengi kama yanavyoonekana pembeni mwa bwawa hili.
Bwawa2

Hii ni aina nyingine ya bwawa lililochimbwa na kujengwa kwa simenti na kulifanya liwe imara zaidi. Nalo lipo katika kituo cha ufugaji wa samaki Kingolwira mjini Morogoro.

 Bwawa3
Bwawa hili limejengwa pia kwa simenti kutoka usawa wa ardhi kwenda juu, ni la mduara kama linavyoonekana kwenye picha hii. Yapo mabwawa mengi ya aina hii katka kituo cha kufugia samaki Kingolwira mjini Morogoro.

Ufugaji wa samaki unamanufaa sana kwa mfugaji kwani unaweza kumuondolea Mtanzania umaskini huku akiendelea kujipatia kitoweo. 
Kuna uhaba mkubwa sana wa samaki Tanzania, ukipita katika masoko ya samaki hasa asubuhi utaona wafanyabiashara wanavyogombania samaki. Hii inaonyesha msisitizo kuwa uhitaji wa samaki Tanzania ni mkubwa na watu wengi wanahitajika kuingia katika ufugaji wa samaki. Itawasaidia kujikwamua kimaisha lakini pia kuwafanya Watanzania wengi wapate kitoweo cha samaki.

 

Leave a Reply