Chakula cha kuku wa mayai

Na Godwin Magambo

Leo nawaletea makala kuhusu utengenezaji wa chakula cha kuku wa mayai (Layers, Kuroilers)

Utengenezaji wa chakula cha kuku kwa kutumia fomyula sahihi ni njia nzuri kwa mfugaji ya kupunguza gharama za mradi wake wa kuku, pia kuhakikisha chakula kinakua na virutubisho muhimu kwa usahihi.

Ifuatayo ni fomyula ya utengenezaji wa chakula cha Kuku: Starter, Grower na Finisher.

——————————

  1. CHICKS STARTER, WIKI 1 – 5
  • Pumba za maindi 41kg
  • Dagaa walio sagwa 5kg
  • Mtama ulio sagwa 25kg
  • Mashudu ya alizeti 22kg
  • Chumvi 0.5kg
  • Damu iliyo sagwa 3kg
  • Unga wa mifupa 2kg
  • Methionine 0.25kg
  • Prexix 0.5kg
  • Vitamins 0.5kg
  • Lysine 0.25kg

TOTAL =100KG

——————————

GROWER MASH, WIKI 6 – 16

  • Mashudu ya alizeti 22kg
  • Ngano nzima 5kg
  • Dagaa walio sagwa 11kg
  • DCP 1kg
  • Unga wa mifupa 5kg
  • Chokaa 2kg
  • Chumvi 0.5kg
  • Mahindi yaliyo parazwa 10kg
  • Premix 0.5kg

TOTAL =100KG

——————————

LAYERS MASH WIKI 17

  • Mashudu ya alizeti 20kg
  • Pumba za mahindi 35kg
  • Chokaa 3kg
  • Mtama 6kg
  • Dagaa walio sagwa 12kg
  • Unga wa mifupa 5kg
  • Damu iliyo sagwa 5kg

——————————

 

Njia rahisi ya kujitengenezea chakula chako nyumbani kwa viambata vinavyopatikana mtaani kwako.

Tengeneza kilo 100 kwa kanuni hizi

 

Chick mash

chakula cha kuku kuanzia siku 1 hadi wiki 8 changanya:

Pumba laini za mahindi kilo 40

Mashudu ya alizeti kilo20

Pumba za mtama kilo 27

Chokaa ya mifugo/unga wa mifupa kilo 2 na robo

Dagaa kilo 10

Chumvi nusu kilo

Premix /broiler premix robo kilo

 

Growers mash miezi 2 – 4

Mahindi yaliyobarazwa kilo 25

Pumba za mahindi kilo 44

Mashudu ya alizeti kilo 17

Chikaa ya mifugo kilo 3 na robo

Dagaa kilo 10

Chumvi robo kilo

Broler premix nusu kilo

 

Growers finisher miezi minne hadi mitano

Mahindi yaliyo barazwa kilo 31

Mashudu ya alizeti kilo 18

Pumba za mahindi kilo 38

Chokaa kilo 2 na robo

Dagaa kilo 13

Brioler premix robo kilo

Chumvi nusu kilo.

 

Kuku wanaotaga miezi 6+

Dagaa kilo 12

Mahindi yaliyo barazwa kilo 30

Mtama kilo 6 na robo tatu

Mashudu ya alizeti kilo 20

Pumba za mahindi kilo 23

Chumvi  robo kilo

Chokaa ya mifugo kilo 3

Unga wa mifupa kilo 5

Layers premix robo kilo

 

MUHIMU

– Hakikisha unachanganya vizuri ili kupata mchanganyiko wenye uwiano Sahihi wa virutubisho.

– Chakula kihifadhiwe vizuri ili kuzuia unyevu.

– Kuku wapewe chakula kwa kiasi kulingana na umri na idadi yao.

Leave a Reply